Msafara wa Uthabiti kati ya Khiyana ya Utawala wa Misri na Wajibu wa Jeshi lake kuchukua Hatua
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Huku kukiwa na mikutano tasa na makongamano ya uhadaifu, msafara maarufu unaojiita "Msafara wa Uthabiti" ulitoka Tunisia, Algeria, na Morocco, kuelekea Gaza kupitia Libya na Misri, kwa lengo la kuvunja mzingiro na kusaidia watu wa Ukanda wa Gaza, ambao wamekuwa chini ya vikwazo kwa zaidi ya miezi kumi na nane. Msafara huo uliwabeba wanaume na wanawake wa rika zote, waliounganishwa kwa lengo moja: kuvunja mzingiro huu uliowekwa na umbile la Kiyahudi kwa watu wa Gaza, kwa ushirika na ushiriki wa moja kwa moja wa tawala zilizo jirani, hasa unaoshikilia bendera kati yao utawala wa Misri.