Jumatano, 22 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/18
Saa hii ni: 05:39:11 (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen Inawapongeza Watu wa Imani na Hekima na Umma wa Kiislamu kwa Sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen inatoa pongezi zake za dhati na baraka zenye thamani kubwa zaidi kwa watu wa imani na hekima, na kwa Amiri wa Hizb, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, na kwa wanachama wote wa Hizb, na kwa Ummah mzima wa Kiislamu kwa sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa mwaka huu wa 1446 H. Mwenyezi Mungu airudishe kwao, juu yetu, na juu ya ulimwengu wote kwa kheri, baraka, na furaha.

Soma zaidi...

Sheria ya Kimataifa ni Sheria ya Pori - Hairuhusiwi Kuiendea

Chini ya ufadhili wa Daniel Capoli, Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu katika misheni ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) nchini Yemen, ICRC huko Sana'a ilipanga, mnamo Jumanne na Jumatano, 20-21/05/2025, kwa ushirikiano na Wizara ya Habari na Wizara ya Mambo ya Nje, kozi ya mafunzo katika Wizara ya Mambo ya Nje kwa wafanyikazi wa vyombo vya habari na taasisi ya waandishi wa habari. Kozi hiyo ilishughulikia sheria za kimataifa, misingi na malengo yake, na istilahi zinazohusiana na sheria za kimataifa za kibinadamu, haswa katika suala la haki za binadamu katika ulinzi na maisha yenye staha, kuzuia ghasia, na kukidhi mahitaji ya vikundi vilivyo hatarini zaidi vinavyofinikwa na ulinzi wake, na vile vile kulinda raia dhidi ya athari za uhasama na kuharamisha mateso yasiyo na haja au madhara kupita kiasi.

Soma zaidi...

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Mahouthi Wanaendelea na Jinai na Uhalifu wao... Kuwakamata Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Kuanzia Alhamisi, tarehe 10 Jumada al-Akhir 1446 H sawia na tarehe 12 Disemba 2024 M, wanamgambo wa Houthi walifanya uvamizi kwenye nyumba za wanachama wa Hizb ut Tahrir bila ya kuzingatia vifungu vya sheria ya Kiislamu au hata kanuni na desturi za kikabila! Walivamia nyumba zao katika kurugenzi tatu za Jimbo la Taiz (Taiziyah, Mawiah, na Khadir); na kuwakamata: Suleiman al-Muhajri, Khaled al-Hami (waliyemwekwa kizuizini miezi sita iliyopita kwa tuhuma za kubeba Dawah pamoja na Hizb ut Tahrir), Mhandisi Taqi al-Din al-Zayla'i, Amir al-Sabry, na Muhammad al-Faqih. Wafuasi watatu wa Hizb ut Tahrir pia walikamatwa: Abdul Malik al-Jundi, Abdul Qader al-Sarari, na Adnan al-Zayla'i, ambao wanasalia chini ya ulinzi wa wahalifu hao mpaka kufikia wakati wa kuandika taarifa hii.

Soma zaidi...

Ala za Kindani kama Kikaragosi cha Makafiri wa Magharibi katika Kutekeleza Sera Zake, na Hakuna Suluhisho kwa Watu wa Yemen isipokuwa kwa Kutekeleza Shariah ya Mwenyezi Mungu

Watu wetu wa Hadhramaut na Yemen yote lazima watambue kwamba uongozi wa kisiasa nchini Yemen, kaskazini na kusini, haujali matatizo na mahitaji yao. Kinyume chake, unazidisha tu mateso yao, iwe kupitia kuzorota kwa uchumi au kukosekana kwa huduma muhimu kama vile umeme, maji, na mahitaji mengine kwa maisha yenye staha. Ni lazima tuondoe uaminifu wetu kutoka kwa wao wote, kwani pindi wanapotenda, huitumikia Magharibi kafiri, na wanaponyamaza, wanapora mali ya nchi na watu wake bila ya uwajibikaji au uangalizi!

Soma zaidi...

Vitendo vya Baraza la Uongozi wa Rais na Serikali yake ni Mithili ya Sarabi Jangwani, na Kuporomoka kwa Sarafu ni Shahidi wa hilo

Sarafu ya nchi katika maeneo yanayodhibitiwa na Baraza la Uongozi wa Rais imeshuhudia mporomoko wa kihistoria dhidi ya sarafu za kigeni kwa wiki kadhaa, huku riyal ya Saudia ikivuka kizuizi cha riyal 535, na dolari ya Marekani ilivuka kizuizi cha riyal 2,000. Wakati huo huo, baadhi ya miji ilishuhudia uasi mdogo wa kiraia na kufungwa kwa maduka ya kupinga kuporomoka kwa sarafu hiyo, na maduka kadhaa ya kubadilisha fedha yalifunga milango yake kwa watu baada ya janga hili la kuporomoka na kutoweza kwa serikali kutafuta suluhisho mwafaka kwa hilo.

Soma zaidi...

Utunzaji nchini Yemen ni Dhaifu kuliko Nyumba ya Buibui!

Mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa mnamo Jumamosi tarehe 31/8/2024 katika wilaya ya Bani Musa Al-Jarf huko Wusab As Safil Wilaya ya Dhamar, yalisababisha vifo vya watu 27, kujeruhiwa kwa watu 8, na kupoteza watu 2. Vyombo vya habari vimeripoti kuwa mafuriko hayo pia yamesababisha kubomolewa kwa nyumba 15, uharibifu wa nyumba 8 katika wilaya ya Wadi Al-Akhshab, na kusombwa kwa magari 4, pikipiki 2 na duka moja.

Soma zaidi...

Kwa kukosekana kwa Mradi wa Kiuchumi wa Mahouthi Kilimo cha Mkataba: Tishio Linalokaribia Kuwasagasaga Wakulima, Kuimarisha Udhibiti wa FAO, na Kushindwa Kufikia Kujitosheleza katika Nafaka nchini Yemen

Mnamo Jumatatu, Agosti 26, 2024, Waziri wa Kilimo, Uvuvi, na Rasilimali za Maji, Dkt. Ridwan Al-Rubai, alifanya mkutano wa mashauriano na wawakilishi wa vyama vya ushirika wa kilimo na wataalam maalum ili kujadili dori muhimu ambayo kilimo cha mkataba kinacheza kama njia madhubuti na ya hali ya juu ya unadi wa bidhaa za kilimo.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu