Jumamosi, 19 Muharram 1448 | 2026/07/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

“Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi.” [Aal-i-Imran: 118]

Chansela wa Ujerumani Friedrich Merz alitangaza mnamo Ijumaa kupinga kwake Muungano wa Ulaya kuweka vikwazo kwa umbile la Kiyahudi, huku Ufaransa ikitangaza kwamba haitakubali kuondoa vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Iran isipokuwa makubaliano yoyote ya mwisho kuhusu mpango wake wa nyuklia yajumuishe kushughulikia mpango wake wa makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wake kwa makundi yenye silaha katika eneo hilo.

Soma zaidi...

Ardhi Zetu Zitabaki Kukiukwa na Damu Yetu Itaendelea Kumwagika Hadi Tutakaposimamisha Khilafah Rashida Yetu

Mnamo Jumapili, tarehe 14 Juni 2026, jeshi la Kiyahudi lilifanya shambulizi la anga likilenga vitongoji vya kusini mwa Beirut, saa chache tu baada ya kuwaonya wakaazi wa takriban miji 30 kusini mwa Lebanon na kuwaamuru waondoke. Tovuti ya habari ya Axios iliripoti kwamba “jeshi la ‘Israel’ liliiarifu CENTCOM muda mfupi kabla ya shambulizi jijini Beirut kutokea.” Trump aliandika kwenye jukwaa lake la ‘Truth Social’ mnamo Jumapili: “Shambulizi la asubuhi ya leo dhidi ya Beirut halikupaswa kutokea, haswa katika siku maalum ambapo tuko karibu sana na Mkataba wa Amani na Iran.”

Soma zaidi...

Serikali ya Tunisia Itaendelea na Uzembe Wake Hadi Lini na Kuruhusu Malori Haya ya Kifo Kuchukua Maisha ya Wafanyikazi wa Kike wa Mashamba?

Ghadhabu na hasira ziliongezeka nchini Tunisia wiki iliyopita kufuatia ajali nyingine mbaya, wakati huu katika wilaya ya Mazouna katika jimbo la Sidi Bouzid. Ajali hiyo iliwaacha wafanyikazi kadhaa wa kike wa shambani wakiwa wamejeruhiwa na wawili wakiwa wamekufa katika eneo la tukio. Tunisia inashuhudia kujirudia kwa matukio kama hayo kutokana na serikali kushindwa kukomesha usafiri usiodhibitiwa na kuboresha hali mbaya ya wafanyikazi wa kike wa mashamba! Bila shaka, serikali hii inakwepa kutoa tarakimu na takwimu sahihi zinazoonyesha ukubwa wa janga hilo!

Soma zaidi...

Moto Mijini: Jinsi Ubepari Unavyowasha Moto katika Miji ya Waislamu yenye Wakaazi Wengi

Mnamo Jumatatu, tarehe 1 Juni 2026, vyombo vya habari viliripoti kuhusu moto mkubwa ulioharibu eneo la makaazi lenye watu wengi huko Kebon Kosong, Kemayoran, Jakarta ya Kati, Indonesia. Takwimu rasmi kutoka kwa Wakala wa Kupunguza Maafa wa DKI Jakarta (BPBD) na uthibitishaji wa uwanjani zinaonyesha takriban familia 354—takriban watu 620—waliachwa bila makao. Takriban watoto 160 wenye umri wa kwenda shule waliathiriwa moja kwa moja.

Soma zaidi...

Je, Erdogan Anasubiri Mayahudi Waipige Mabomu Ankara Kabla ya Kuhamasisha Jeshi Lake?!

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba aliyotoa wakati wa mkutano wa kundi la wabunge wa Chama cha Haki na Maendeleo katika Bunge la Uturuki, alisema: "Tunafahamu vyema lengo kuu la udanganyifu wa 'Ardhi iliyo Ahidiwa', na Mungu akipenda, hatutaruhusu kamwe." Alifafanua kwamba usalama wa Uturuki hauanzii katika mkoa wa Hatay kusini mwa Uturuki, bali Aleppo, Damascus, na Beirut. Aliendelea: "Ikiwa uonevu wa Israel hautasimamishwa, gharama haitalipwa na eneo hilo pekee, bali na wanadamu wote." Erdoğan alizisihi dola kuu duniani kuchukua msimamo wazi dhidi ya umbile hilo la Kizayuni, akisema: "Kuirudisha Israel katika kufuata sheria sio tena jukumu la baadhi ya nchi tu, bali ni jukumu la pamoja linalowaangukia wanadamu wote."

Soma zaidi...

Mtoto Aliyeuawa Shahidi, Kuhesabiwa kwa Waathiriwa Kutaisha Lini? Watu wa Damu hiyo Watainuka Lini Kuwalipiza Kisasi?

Wizara ya Afya ya Palestina ilisema kwamba vikosi vya uvamizi vilifyatua risasi kwenye gari moja lililokuwa limebeba raia wa Palestina katika mji wa Hebron katika Ukingo wa Magharibi wa kusini unaokaliwa kimabavu, na kusababisha kifo cha kishahidi cha mtoto mchanga wa miezi saba Sam Abu Hikal huku akiwa mikononi mwa mamake. Mamake na babake pia walijeruhiwa.

Soma zaidi...

Ulaya Yahangaika Siku Chache Tu Bila Mafuta na Gesi ya Waislamu: Vipi Basi Ikiwa Ummah Ungeamka?!

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Roland Lescure alisema kwamba serikali haziwezi kuamua kama zitoe akiba ya ziada ya mafuta ya kimkakati ili kupunguza usumbufu unaosababishwa na vita vya Iran hadi muda unaowezekana wa mzozo huo utakapokuwa wazi. Katika muktadha huo huo, mashambulizi ya awali ya makombora ya Iran kwenye kituo cha gesi cha Ras Laffan nchini Qatar, mojawapo ya vituo vikubwa zaidi vya gesi asilia vilivyoyeyushwa duniani, yalisababisha kupungua kwa kasi kwa akiba ya gesi ya Uingereza. Akiba ya gesi asilia nchini Uingereza ilishuka hadi viwango vya kutosha kukidhi matumizi ya ndani kwa muda usio zidi  masaa 48.

Soma zaidi...

Pongezi kwa Idd ul-Adha Iliyobarikiwa 1447 H

Kutoka kwa Mtume (saw) ambaye amesema: «إِنَّ أَعْظَمَ الْأَيَّامِ عِنْدَ اللهِ يَوْمُ النَّحْرِ» “Hakika siku tukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni siku ya Arafah”, basi kwa mnasaba huu uliobarikiwa na kwa kutukuza alama za Mwenyezi Mungu Azza wa Jalla: ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ﴿ “Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo.” [Al-Hajj: 32], na Licha ya majanga ambayo Umma wa Kiislamu unapitia chini ya watawala waliouangusha na kuusalimisha kwa adui yake, ambayo yamejaza nyoyo zetu maumivu na huzuni, bado tunapaswa kutoa pongezi na baraka zetu za dhati kwa Umma wetu wa Kiislamu, wenye subira, na wenye kutaraji mema katika Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu azifanye siku hizi za Idd kuwa za baraka, ushindi, na kuinuliwa.

Soma zaidi...

Je, Sio Wakati wa Ummah Kuwekeza Utajiri Wake Katika Kujenga Maslahi na Nguvu Zake Wenyewe?

Utajiri na rasilimali za Ummah zinaendelea kufujwa ili kutajirisha Magharibi, huku ndani ya nchi, zikitumika kwa anasa zinazowaweka Waislamu mbali na mfumo wa maisha wa Kiislamu. Mnamo Alhamisi, 21/5/2026, Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia ilitangaza muungano mpya wa Saudi Arabia na Misri unaolenga kujenga mfumo jumuishi wa matukio makubwa katika eneo hilo, unaounganisha nchi hizo mbili kwenye njia moja ya kuvutia wasanii na nyota wa kimataifa! Wakati huo huo, mnamo Jumatano, 20/5/2026, nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba (GCC) na Uingereza zilitangaza makubaliano ya kihistoria na makubwa ya biashara huria yenye thamani ya takriban dolari bilioni 5, na kuifanya Uingereza kuwa taifa la kwanza la G7 kusaini makubaliano kama hayo na kambi ya Ghuba.

Soma zaidi...

Msikose Fursa ya Kuunda Mfumo Mpya wa Kimataifa, Enyi Waislamu — Nyinyi Ndio Watu Wake na Mnaliweza hilo Kupitia Itikadi Yenu Tukufu

Hivi majuzi, Rais wa Urusi Vladimir Putin alitembelea China, na mwishoni mwa ziara hiyo taarifa ya pamoja ya zaidi ya nukta arubaini ilitolewa. Ndani yake, nchi hizo mbili zilitangaza mikataba na makubaliano kadhaa. Hata hivyo, kinachoonekana katika taarifa hiyo ni wito wa nchi zote mbili wa mpangilio mpya wa ulimwengu wa nchi nyingi. Pia inaeleweka kwamba ziara ya Putin nchini China ilikuja baada ya ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump nchini China, na baada ya ziara ya Putin kukamilika ilitangazwa kwamba rais wa China anakusudia kutembelea Korea Kaskazini.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu