Jumamosi, 19 Muharram 1448 | 2026/07/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Malaysia: Hati ya Pingamizi kuhusu “KL Headline Msimu wa 2026”

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Malaysia (HTM) uliwasilisha hati ya pingamizi kwa Wizara ya Mawasiliano huko Putrajaya kuhusu kuandaliwa kwa tamasha la “KL Headline Msimu wa 2026”. Hatua hii ilichukuliwa ili kuihimiza serikali kufuta tamasha hilo mara moja, kutokana na madhara makubwa ambayo lingesababisha kwa jamii na ukiukaji wake wa wazi wa sheria ya Kiislamu. Hati hiyo ilipokelewa na Bi. Wan Saidatul Shafina binti Mohamed Amin, Katibu wa Idara ya Mawasiliano ya Kimkakati na Masuala ya Taasisi, kwa niaba ya Wizara. Pia alitenga muda wa kusikiliza maelezo kamili na ya kina ya sababu za pingamizi zilizowasilishwa na Hizb ut Tahrir Malaysia.

Soma zaidi...

“KL Headline Msimu wa 2026”: Serikali ya Madani Haijali tena Ghadhabu ya Mwenyezi Mungu!

Kuala Lumpur iko tayari kuibuka kama mahali mwanana pa ziara za matamasha ya kimataifa barani Asia kupitia “KL Headline Msimu wa 2026,” ambao unakutanisha maonyesho 25 ya wasanii wa kimataifa katika mwaka mzima wa 2026. Mji mkuu wa Malaysia umepangwa kuwa mwenyeji wa maonyesho 25 ya wasanii wa kimataifa katika maeneo sita, yakiwalenga zaidi ya mashabiki 500,000 kutoka pwani za ndani na nje ya nchi - kulingana na mratibu, Live Nation Malaysia.

Soma zaidi...

Kuikaribisha Ziara ya Modi: Khiyana ya Wazi kwa Damu na Heshima ya Umma wa Kiislamu

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi amepangwa kufanya ziara ya kikazi nchini Malaysia mnamo Februari 7-8, 2026, na inaripotiwa kwamba anatarajiwa kupokea mapokezi makubwa kutoka kwa serikali na jamii ya Mabaniani nchini Malaysia. Kibaraka huyu wa Amerika mara nyingi hupokea mapokezi ya heshima katika nchi nyingi kote duniani na hupewa tuzo nyingi na nchi anazotembelea, wakiwemo watawala Ruwaibidha wa Waislamu, kiasi kwamba baadhi wako tayari kukita masanamu ili tu kumfurahisha kiongozi huyu mshirikina.

Soma zaidi...

Unafiki wa Kisiasa katika Demokrasia Kamwe Hautaisha Mpaka Tuubadilishe kwa Siasa za Kiislamu

Mnamo tarehe 06/01/2025, rufaa ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Najib Tun Razak kuhusu kuwepo kwa amri ya nyongeza ya Mfalme, inayomruhusu kutumikia kifungo chake kilichosalia chini ya kifungo cha nyumbani, imekubaliwa na mahakama kwa wingi wa 2-1. Majaji wa Mahakama ya Rufaa kisha wakaamuru kesi hiyo irudishwe katika Mahakama Kuu ili ombi la Najib la uhakiki wa mahakama lisikizwe na jaji mpya. Amri hii ya nyongeza, ambayo ni sehemu ya mchakato wa msamaha wa kifalme, imekuwa jambo la kawaida, ambalo halijawahi kutokea katika asili yake. Sambamba na hilo, kulikuwa na jambo jengine - mkusanyiko mkubwa wa kuonyesha mshikamano uliokusanyika nje ya mahakama, ulioandaliwa na vyama ambavyo hapo awali vilikuwa wapinzani wa kisiasa wa Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Soma zaidi...

Miaka Miwili ya Utawala bila Uislamu: Kupuuza Amana ya Mwenyezi Mungu

Katika hafla ya kuadhimisha mwaka wake wa pili afisini, Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim, aliandaa Mpango wa Miaka Miwili wa Serikali ya Madani (2TM) na Kongamano la Kitaifa la 2024 la Marekebisho ya Utumishi wa Umma mnamo Novemba 23-24, 2024 katika Jumba la Mikutano la Kuala Lumpur (KLCC). Hafla hilo ilionyesha huduma mbalimbali za serikali chini ya paa moja, na zaidi ya vibanda 30 vinavyotoa huduma na bidhaa kwa umma. Ripoti zilisifu hafla hiyo kuwa ya mafanikio, ikiwa na zaidi ya wageni 200,000. Zaidi ya hayo, Anwar aliendesha kikao cha ukumbi wa jiji kuangazia mafanikio na mipango yake chini ya serikali ya Madani huku akishughulikia ukosoaji, haswa kuhusu mahojiano yake ya CNN yenye utata kuhusu uwepo wa umbile la Kiyahudi na ufadhili wa makampuni ya kibinafsi wa safari zake na ujumbe wake nje ya nchi.

Soma zaidi...

Baada ya Mwaka Mmoja wa Mauaji ya Halaiki (na Miaka 76 ya Ukaliaji Kimabavu), Watawala wa Ruwaibidha Wakusanyika Tena Kuendeleza Kejeli na Usaliti wao

Ni mwaka mmoja kamili baada ya watawala wa Waarabu na Waislamu kukusanyika kujadili kadhia ya Palestina kufuatia mkasa wa Oktoba 7, wanakutana tena mahali pale pale, pamoja na mtu yule yule, wakishughulikia tatizo lile lile, na hatimaye kutoa maazimio yale yale! Zaidi ya viongozi 50 wa dola za Waislamu walihudhuria Mkutano wa Waarabu na Waislamu mnamo tarehe 11/11/2024, akiwemo Waziri Mkuu wa Malaysia. Kwa kutabiriwa, mapendekezo yaliyochakaa yaliwasilishwa, na Mkutano huo ulihitimishwa kwa maazimio yaliyochakaa vilevile. Kikubwa kinachotolewa na watawala hao ni kulaani mauaji ya halaiki ya Gaza na ‘Israel’ na kuomba Umoja wa Mataifa (UN) - shirika lile lile lililohusika na kuzaliwa kwa umbile halifu la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Demokrasia Humpa Mwanadamu, Wakiwemo Wasiokuwa Waislamu, Uwezo wa Kufafanua na Kubainisha Imani na Madhehebu Yetu!

Pendekezo la hivi majuzi la Mswada wa Sheria ya Mufti 2024 (Maeneo ya Shirikisho) limezua mjadala mkali kote nchini Malaysia. Tangu kusomwa kwake kwa mara ya kwanza mwezi Julai, Mswada huo umesonga mbele, ukikaribia kusomwa mara ya pili na ya tatu kabla ya kuidhinishwa kamili na bunge. Mwanzo wa Mswada huu unatokana na mjadala unaoendelea kuhusu Ilm al-Kalam (Usomi wa Kiislamu), ambao umeongezeka hivi karibuni nchini Malaysia.

Soma zaidi...

Ikiwa Sera ya Mambo ya Nje ni Kufanya Urafiki na Adui, Basi Ziara ya Adui Hakika Itakaribishwa!

Inasikitisha kwamba Malaysia inaendelea kudumisha uhusiano wa kidiplomasia na China (na pia Urusi), licha ya ukatili uliothibitishwa na ukandamizaji unaofanywa na nchi hiyo ya kikomunisti dhidi ya Waislamu wa Uighur kwa miongo kadhaa. Mbali na uhusiano wa kidiplomasia, Malaysia pia imeanzisha uhusiano mkubwa wa kibiashara na China, na kuifanya kuwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa nchi hiyo.

Soma zaidi...

Umepita Mwaka Tangu Mauaji ya Gaza Huku Watawala wa Waislamu Wakisalia kama Watazamaji. Hakika Suluhisho Moja na la Pekee ni Khilafah!

Enyi Waislamu, kwa kuzingatia kimya cha watawala wote na vikosi vyao vya majeshi, tunasisitiza kwamba suluhisho pekee la ukombozi wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina ni kusimamishwa Khilafah. Hizb ut Tahrir inakulinganieni kwa dhati na bila kuchoka kushiriki katika kazi hii tukufu na ya dharura. Muna khiari ya ima kunyamaza, kuendelea kuwaunga mkono watawala wenu, au kuungana mikono na Hizb ut Tahrir katika kazi zetu za kuregesha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu