Jumamosi, 21 Rajab 1447 | 2026/01/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah... Dunia Inajitayarisha Kurudi Kwake

Mtu anaweza kufikiri, huku akiangalia yanayojiri hivi karibuni katika ngazi ya kimataifa na katika ardhi za Kiislamu, kwamba uhalisia unazidi kuwa wa giza tororo kwa Umma wa Kiislamu, na kwamba matumaini ya kuamka kwake na kuregeshwa kwa heshima yake yanafifia au kupungua. Hata hivyo, kutafakari haya yanayojiri kunaonyesha kwamba yanafichua matumaini ambayo yanajajidishwa na kuzidi kuwa makubwa, na mbinu ya kuelekea mwamko siku baada ya siku.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Yafanya Mikutano Kadhaa katika Miji mbalimbali nchini Sudan

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, mnamo Rajab 1342 H, na kuukumbusha Ummah kuhusu tukio la kusikitisha lililosababisha Ummah kumpoteza Imam wake, ngao, umoja wake kuvunjika, na kafiri mkoloni kuutawala, kudhibiti maamuzi yake ya kisiasa, kiuchumi, na kijeshi, na kuhamasisha Ummah kufanya kazi ya kuregesha maisha kamili ya Kiislamu kupitia kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume

Soma zaidi...

Pindi Uwakilishi Unapokuwa Badali ya Wahyi

Kuapishwa kwa Zohran Mamdani mnamo tarehe 1 Januari 2026, kama wengi kabla yake, kunasherehekewa kama hatua muhimu kwa “uwakilishi wa Waislamu” ndani ya demokrasia ya Magharibi. Hata hivyo, zaidi ya siasa za nembo na utambulisho kuna swali zito zaidi, ambalo linagusa msingi wa itikadi ya kisiasa ya Uislamu: Je, inaruhusiwa kwa Muislamu kushikilia wadhifa wa utunzi wa sheria?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah (Rajab 1342 - Rajab 1447 Hijri)

Sisi katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan tunafuraha ya kuwakaribisha wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wenye hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Umma cha kila mwezi, ambacho mwezi huu kitakuwa na kichwa: Khilafah Ilivunjwa, na Afya ya Watoto Wetu Ikakiukwa

Soma zaidi...

Kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105, Tunaufufua Wito kwa Majeshi Yote ya Ummah Kuhamasisha Nguvu Zao Ili Kusimamisha Khilafah Rashida

Mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na tarehe 3 Machi, 1924 M, amri ovu ilitolewa na lile lililoitwa Bunge Kuu la Kitaifa, ikielezea kufutwa rasmi kwa Khilafah. Kwa kuvunjwa kwa Khilafah, hukmu za Sharia ziliondolewa, kiapo cha utiifu (Bay’ah) kilisitishwa, na ardhi za Waislamu zilichanwa vipande vipande kwa misingi ya kitaifa na kikabila kuwa vijidola tete, tegemezi, na dhaifu. Vibaraka wa kulipwa waliteuliwa kuzitawala. Fikra ya umoja ilipigwa pigo kubwa. Kwa kuangamia kwake, Bayt al-Maqdis na Ardhi Iliyobarikiwa zilianguka, na umbile lenye saratani la Kiyahudi lilipandwa katikati ya ardhi za Waislamu.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafurahi kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo mgeni atakuwa ni Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil) – Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan – chenye kichwa: Kwa Mnasaba Kumbukumbu ya Kuvunjwa kwa Khilafah (Ukhalifa): Kusimamishwa kwake tena ni Faradhi ya Sharia

Soma zaidi...

Hofu Halisi ya Magharibi: Ulimwengu wa Kiislamu Ulioungana

Katika mahojiano ya hivi karibuni ya Fox News na Sean Hannity, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio alifufua usemi maarufu wa “Uislamu wenye msimamo mkali,” Khilafah inayopanuka, na vitisho kwa Magharibi. Maoni yake hayarudii tu miongo miwili ya ujumbe wa baada ya 9/11 lakini pia yanafichua jambo la kina zaidi - hofu ya msingi ya ulimwengu wenye nguvu wa Kiislamu ulioungana.

Soma zaidi...

Hotuba ya Mwanachuoni na Amiri wa Hizb ut Tahrir Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah (Mwenyezi Mungu amlinde) Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Katika siku hizi kama hizi, miaka 105 iliyopita, mwishoni mwa Rajab 1342 H, sambamba na mapema Machi 1924 M, wakoloni makafiri, wakiongozwa na Uingereza wakati huo, kwa ushirikiano na wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, waliweza kuivunja Khilafah. Mhalifu wa zama hizo, Mustafa Kemal, alitangaza ukafiri wa wazi kwa kuifuta Khilafah, kumzingira Khalifa jijini Istanbul, na kumfukuza alfajiri siku hiyo hiyo. Hivyo, tetemeko baya la ardhi lilizikumba ardhi za Waislamu kwa kuvunjwa Khilafah, chimbuko la izza yao na radhi ya Mola wao Mlezi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu