Alhamisi, 23 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/19
Saa hii ni: 11:35:02 (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ni Nani atakayewatetea Wanawake wa Sudan na Darfur?

Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (Médecins Sans Frontières) limeonya kuwa wanawake na wasichana katika jimbo la Darfur nchini Sudan wako katika hatari ya karibu kila mara ya unyanyasaji wa kijinsia. Mizani halisi ya mgogoro huu inasalia kuwa vigumu kubainisha, kwani huduma bado ni chache na watu wanakabiliwa na vikwazo katika kutafuta matibabu au kuzungumza kuhusu masaibu yao. Hata hivyo, manusura wote waliozungumza na timu za MSF huko Darfur na kuvuka mpaka nchini Chad walisimulia hadithi za kutisha za ghasia za kikatili na ubakaji. Huku wanaume na wavulana pia wakiwa hatarini, kiwango cha mateso kinapita maelezo.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu! Msidharau Matendo Yenu Wenyewe kwa Kuangalia Matendo ya Watu! Kwa sababu Nyinyi Ni “Mashahidi” Juu ya Wanadamu!

Meli ya misaada ya "kwenda Gaza" ya Madleen na matendo ya wanaharakati wake maarufu wasio Waislamu yamekuwa na athari kubwa kwenye vyombo vya habari vya kawaida na mitandao ya kijamii. Nchi nyingi, ikiwemo Uturuki, zilitoa "msaada wa ushauri" kwa raia wao wenyewe kwenye meli hiyo, ambayo ilikamatwa na umbile vamizi la kigaidi la kizayuni.

Soma zaidi...

Utelekezaji wa Serikali ya Misri wa Gaza: Kuanzia Kuzuia Nusra, Hata wa Maneno, hadi Kushiriki kwa Kizuizi!

Katika mandhari inayojirudia rudia, kwa kila maafa yanayowakumba watu waliozingirwa wa Gaza, tawala za Kiarabu - zinazoongozwa na utawala wa Misri - zinathibitisha kwamba sio tu hazipo katika wajibu wao wa kunusuru, lakini pia ziko katika nafasi ya ulaji njama na usaliti, na hata kushiriki kikamilifu katika mzingiro, kulinda vivuko na kuzuia mradi wowote wakilishi au maarufu kwa lengo la kukandamiza Waislamu.

Soma zaidi...

Tahadharini kwamba Kuondelewa Vikwazo vya Marekani kunaweza kuwa Utangulizi wa Kupoteza Ubwana na Utangulizi wa Uhalalishaji Mahusiano na Mayahudi

Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa alikutana na mwenzake wa Marekani, Donald Trump, katika mji mkuu wa Saudi, Riyadh, mnamo Jumatano, kando ya mkutano wa kilele wa Ghuba na Marekani. Mfalme matarajiwa wa Saudia Mohammed bin Salman alihudhuria mkutano huo, huku Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan akishiriki kwa njia ya video, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Saudia.

Soma zaidi...

Kongamano la Amani ya Kiraia jijini Damascus Utangulizi wa Kuwaondoa Watiifu wa Serikali na Kuhalalisha Nembo za Ukandamizaji na Uhalifu

Mkutano na waandishi wa habari uliofanywa na Kamati ya Amani ya Kiraia katika jengo la Wizara ya Habari jijini Damascus mnamo Jumanne, Juni 10, 2025, chini ya uenyekiti wa mwanakamati Hassan Soufan, ulizua wimbi kubwa la hasira na chuki kubwa miongoni mwa Wasyria, hasa miongoni mwa familia za mashahidi na waliopotea, na watoto wa mapinduzi. Wengi waliona kauli za mkutano huo kama uchochezi kwa familia za wahasiriwa, kupuuza mihanga ya wanamapinduzi, kudharau damu ya mahsahidi, kukana ukweli usiopingika, na uhalalishaji wa wazi wa wahalifu wa kivita. Hafla hiyo ilionekana kama jaribio la kulalalisha mahusiano kwa nembo za utawala ulio ng’atuliwa chini ya mabango ya "amani ya raia," "kujenga taifa," na "kuzuia umwagaji damu."

Soma zaidi...

Utawala wa Jordan Unalilinda Umbile Adui la Kiyahudi kwa Kuyapangua Makombora na Droni Zinazoelekezwa kwake

Mnamo siku ya Ijumaa, tarehe 13/6/2025, alfajiri, umbile la Kiyahudi lilianzisha mashambulizi dhidi ya Iran, yakilenga vituo vyake vya nyuklia, viwanda vyake vya makombora ya balestiki, na viongozi wa kijeshi, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa maisha na mitambo ya kijeshi na ya kiraia, kwa msaada na ushirikiano wa Marekani. Iran, kama kawaida, iliapa kutoa jibu kali na baya kwa umbile la Kiyahudi kupitia mashambulizi ya droni na makombora. Ilitekeleza mawimbi ya mashambulizi haya asubuhi na jioni ya siku hiyo hiyo, yakivuka anga ya Iraq, Syria, na Jordan. Baadhi ya mashambulizi haya yalisababisha uharibifu kwa baadhi ya vifaa katika miji ya umbile hilo, kabla ya baadhi yake kupanguliwa katika anga ya jirani kabla na baada ya kufika kwenye umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Afisi ya NATO nchini Jordan: Kujisalimisha kwa Nchi na Kuahidi Kutumikia Maslahi ya Kikoloni ya Maadui wa Ummah

Mnamo siku ya Alhamisi, 12 Juni 2025, Jordan na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) walitia saini makubaliano jijini Brussels ili kuwa mwenyeji wa afisi ya mawasiliano ya kidiplomasia ya muungano huo katika mji mkuu, Amman. Makubaliano hayo yalitiwa saini kwa niaba ya Jordan na Balozi Yusuf Bataineh, balozi aliyeidhinishwa katika NATO, na kwa niaba ya muungano huo na Javier Colomina, Mwakilishi Maalum wa NATO kwa jirani wa Kusini, ambaye alisifu uhusiano uliotukuka na Jordan na kuthamini ukaribishaji wa afisi ya Jordan na dori yake kuu katika kanda, akiizingatia kuwa mshirika wa kutegemewa kwa muungano huo katika nyanja tofauti tofauti.

Soma zaidi...

Kuna Uungwana kutoka Ng'ambo ya Bahari... Uko wapi Uungwana wa Jeshi la Misri?!

Katika wakati ambapo mauaji dhidi ya watu wa Gaza yamezidi, na ardhi kuungua chini ya miguu ya wanyonge, vyombo vya habari vya Marekani vimeandika kichwa cha kikuu habari kuhusu kijana Muislamu kutoka Misri aitwaye Mohammed Sabry Soliman, ambaye alituhumiwa kwa kurusha vinywaji vya Molotov kwenye maandamano ya kuunga mkono umbile la Kiyahudi nchini Amerika, akiimba "Uhuru kwa Palestina." Wakati vyombo vya habari vinajadili tukio hili, kiini cha tukio hili hakiwezi kupuuzwa: kijana Muislamu, aliyehama kutoka ng'ambo ya bahari, akisukumwa na maumivu ya moyo wake na maumivu ya Ummah wake, kueleza kukataa kwake kimya cha kimataifa na kufeli kwa Waarabu kushughulikia hali inayoendelea mjini Gaza.

Soma zaidi...

Pongeza kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq kwa Sikukuu ya Idd al-Adha 1446 H

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq inatoa pongezi na baraka zake nyingi kwa Umma wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Hasa tunatoa salamu hizi kwa wabebaji da’wah, na kwa mwanachuoni mkubwa, Amiri wa Hizb utTahrir, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah Mwenyezi Mungu amlinde na amhifadhi na ampe ushindi na tamkini kupitia mikono yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir Ndio Inayofanya Kazi Ipasavyo Kusimamisha Khilafah Basi Acheni Kuvuruga Ulinganizi Wake na Kuwakamata Wanachama Wake

Tangu kuanzishwa kwake kama chama cha kisiasa chenye msingi wa Uislamu mwaka 1953, Hizb ut Tahrir imefanya kazi ya kurudisha mfumo kamili wa Kiislamu wa maisha ya Kiislamu kupitia kusimamisha dola ya Kiislamu, ambayo dola yake ya kwanza ilianzishwa na Mtume Muhammad (saw) mjini Madina. Ingawa inafuata njia ya Mtume (saw) ya kusimamisha dola hii, haijishughulishi na kitendo chochote cha kinguvu au kile kinachoitwa vurugu katika kufanya hivyo.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu