Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 581
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mtu anaweza kufikiri, huku akiangalia yanayojiri hivi karibuni katika ngazi ya kimataifa na katika ardhi za Kiislamu, kwamba uhalisia unazidi kuwa wa giza tororo kwa Umma wa Kiislamu, na kwamba matumaini ya kuamka kwake na kuregeshwa kwa heshima yake yanafifia au kupungua. Hata hivyo, kutafakari haya yanayojiri kunaonyesha kwamba yanafichua matumaini ambayo yanajajidishwa na kuzidi kuwa makubwa, na mbinu ya kuelekea mwamko siku baada ya siku.
Katika siku hizi kama hizi, miaka 105 iliyopita, mwishoni mwa Rajab 1342 H, sambamba na mapema Machi 1924 M, wakoloni makafiri, wakiongozwa na Uingereza wakati huo, kwa ushirikiano na wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, waliweza kuivunja Khilafah. Mhalifu wa zama hizo, Mustafa Kemal, alitangaza ukafiri wa wazi kwa kuifuta Khilafah, kumzingira Khalifa jijini Istanbul, na kumfukuza alfajiri siku hiyo hiyo. Hivyo, tetemeko baya la ardhi lilizikumba ardhi za Waislamu kwa kuvunjwa Khilafah, chimbuko la izza yao na radhi ya Mola wao Mlezi.
Katika mwezi mtukufu wa Rajab wa mwaka huu, 1447 H (2026 M), tunakumbuka kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Kiislamu na wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, vibaraka wa wakoloni makafiri. Dola hii ilianzishwa na Bwana wa Mitume, Muhammad (saw), na Maswahaba zake Watukufu (ra). Mfumo wa utawala wa Kiislamu (Khilafah) uliondolewa mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na 3 Machi 1924 M, mikononi mwa mhalifu Mustafa Kemal.
Kutoka ukurasa huu, tutaangazia amali zilizoandaliwa na Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab Tukufu 1342 H.
Mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na tarehe 3 Machi, 1924 M, amri ovu ilitolewa na lile lililoitwa Bunge Kuu la Kitaifa, ikielezea kufutwa rasmi kwa Khilafah. Kwa kuvunjwa kwa Khilafah, hukmu za Sharia ziliondolewa, kiapo cha utiifu (Bay’ah) kilisitishwa, na ardhi za Waislamu zilichanwa vipande vipande kwa misingi ya kitaifa na kikabila kuwa vijidola tete, tegemezi, na dhaifu. Vibaraka wa kulipwa waliteuliwa kuzitawala. Fikra ya umoja ilipigwa pigo kubwa. Kwa kuangamia kwake, Bayt al-Maqdis na Ardhi Iliyobarikiwa zilianguka, na umbile lenye saratani la Kiyahudi lilipandwa katikati ya ardhi za Waislamu.
Katika kumbukumbu ya mapinduzi, Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia, katika eneo la Sidi Bouzid, iliandaa semina yenye kichwa “Na Mapinduzi Yanaendelea...”