Hali Imefikia Hatua Ambapo Watawala wa Waislamu Wanacheza Kamari na Hatari ya Nyuklia Katikati ya Ardhi za Waislamu!
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Afisi ya Habari ya Abu Dhabi iliripoti kwamba timu maalum za kukabiliana na dharura mnamo Jumapili zilidhibiti moto uliozuka katika jenereta ya umeme iliyoko nje ya eneo la ndani la Kiwanda cha Nguvu za Nyuklia cha Barakah katika eneo la Al Dhafra, kufuatia shambulizi la droni kwenye eneo hilo, bila majeraha yoyote au uvujaji wowote wa mionzi uliorekodiwa. Wizara ya Ulinzi ya Imarati ilieleza kwamba uchunguzi bado unaendelea ili kubaini chanzo cha mashambulizi hayo, ikibainisha kuwa maendeleo yoyote yatatangazwa mara tu uchunguzi utakapokamilika.



